BEKI, Mbrazili David Luiz, anasema kwamba anaondoka Chelsea
akiwa na masikitiko makubwa. Staa huyo amefuzu vipimo vya afya na
kufikia makubaliano binafsi na klabu ya Paris Saint-Germain kwenye
uhamisho wake uliowagharimu mabingwa hao wa Ufaransa Pauni 50 milioni.
Uhamisho huo unamfanya Luiz kuwa beki ghali zaidi
duniani na kuvunja rekodi za mabeki wengine kadhaa waliowahi kuhamishwa
kwa pesa nyingi kwenye mchezo huo wa soka.
Ilichokifanya PSG ni kama Real Madrid ilipovunja
rekodi ya Cristiano Ronaldo ya Pauni 80 milioni kwa kumnunua Gareth Bale
kwa Pauni 86 milioni baada ya mabeki waliokuwa wakishikilia rekodi ya
kuwa ghali duniani ni Marquinhos na Thiago Silva.
Luiz apandiwa ndege
Baada ya Chelsea kukubali kufanya biashara na PSG,
mabosi wa klabu hiyo tajiri ya Ufaransa iliwapandisha ndege wawakilishi
wake nchini Brazil kwenda kumpima afya Luiz ili kukabilisha dili hilo.
Tukio hilo hilo lilifanyika Ijumaa iliyopita
wakati Luiz alipokuwa kwenye kambi ya timu ya taifa ya Brazil
inayojiandaa na fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika kwenye ardhi
ya nchi hiyo kuanzia mwezi ujao.
Baada ya klabu ya Chelsea kuthibitisha kupitia
kwenye tovuti yake kwamba imemuuza Luiz, staa huyo Mbrazil alifichua
kuumia kwa uhamisho huo kwa sababu aliishi Stamford Bridge kwa karibu
miaka minne na amezoea sana mahali hapo.
“Nawashukuru Chelsea kwa kipindi chote za miaka mitatu na nusu niliyokaa mahali hapo. Nimepata ushirikiano mkubwa sana.
Nawashukuru wachezaji wenzangu, mabosi na
mashabiki. Naondoka kwa huzuni kubwa, lakini pia nafurahia changamoto
hii kwa kujiunga na klabu kubwa na inayojaribu kujipanga zaidi,”
alisema.
PSG inaamini kwamba imemnasa moja ya mabeki wa
maana sana duniani na kwamba itaendelea kutumia pesa kusajili wakali
wengine baada ya fainali za Kombe la Dunia.
Mabeki wengine ghali
Uhamisho wa Luiz unavunja rekodi za uhamisho ghali
wa mabeki wengi sana na kwenye orodha hiyo wamo, Thiago Silva aliyehama
AC Milan kwenda PSG kwa Pauni 35.3 milioni, Marquinhos (Roma kwenda
PSG) kwa pauni 30.1 milioni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni